Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +25565373432 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

About Ubungo Scout



CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA 
WILAYA YA UBUNGO
1.1.         Utanngulizi.
Chama cha skauti ni chama cha kielimu  chenye malengo ya kumkuza kijana kiimani, kiakili, kijami na kimwili kupitia shughuli mbali mbali kwa kutumia mbinu za kiskauti (scout methods) ili kuijenga dunia iliyo bora  zaidi (creating a better world). Skauti ni chama cha malezi ya vijana, hakihusiani na vyama vya siasa wala dini  na nichama kinachotoa elimu isiyo rasm (non-formal education).

Ni chama cha kielimu cha  hiari na cha kujitolea  kwa vijana wote bila ubaguzi wa aina yoyote ile yaani rangi, kabila, jinsi , dini  au  itikadi. Chama cha skauti Tanzania kilianzishwa mwaka 1912 kikiwa na lengo lile lile la kumwandaa   kijana kielimu  na kumfanya aweze kujitegemea  na aweze kukabiliana na changamoto mbalimbali anazokumbana nazo katika jamii  inayomzunguka   na kuzitatua  na kuwa msaada  wa kutegemewa na jamii husika.

Lengo la skauti ni kuchangia Elimu ya kijana kwa kuiongezea thamni kupitia Ahadi na kanuni za skauti, lakini pia kusaidia kuifanya dunia kuwa mahala bora kwa kuishi Ili kufikia lengo kuu la Skauti”Creating a better World – Kuifanya Dunia kuwa Bora”, Uskauti huendeshwa kwa kuzingatia mbinu kuu saba ambazo kwa wengine hueleweka kama mfumo endelevu wa kujifunzia / kufundishia (Youth program/progressive scheme) ambao Skauti hutumia.

1.2.          Uongozi wa Skauti ngazi ya Wilaya
Chama cha skauti ngazi ya wilaya kilipata uteuzi wa kwanza wa kamishna na msaidizi wake mnamo mwaka 2017 mwezi July tangu kuanzishwa kwa Wilaya mpya ya Ubungo (2015) na kuapishwa rasmi mkoani Dodoma katika maadhimisho ya miaka 100 ya Skauti nchini. kadhalika mwaka huu 2019 mwezi March Kamishna Mkuu alifanya uteuzi mpya wa makamishna wakuu wasaidizi pamojana makamishna wa Mikoa na Wilaya, hivyo aliteua Kamishna na Kamishna Msaidizi wa Wilaya yetu hii ya Ubungo na kuapishwa rasmi katika ofisi za Makao Makuu ya chama cha Skauti – Upanga amabao ni Bw. Florence J. Assenga – Kamishna wa Wilaya na Bw. Murtadhwa R. Abdallah – Kamishna Msaidizi wa Wilaya. Kama kawaida  utaratibu ulivyo ,Uongozi  wa Wilaya tumeunda kamati ya Uendeshaji yenye waratibu takriban 13 katika idara mbali mbali, ili kuunganisha nguvu zetu kwa lengo la kuendeleza Skauti kwa ufanisi mkubwa  katika  Wilaya  yetu ya Ubungo.

Bodi ya Skauti ya Wilaya ndiyo chombo kinachosimamia shughuli za Skauti Wilaya ya Ubungo kwa niaba ya Baraza la Skauti Taifa, ambapo kwa sasa bado tunaitumia bodi iliyoundwa awali hadi hapo itakapo fikia wakati wa kufanya uchaguzi mpya wa Bodi nyengine kwa mujibu wa katiba ya chama cha Skauti Tanzania.

1.3.         IDARA MBALIMBALI ZA CHAMA NGAZI YA WILAYA - UBUNGO

1.3.1.      Idara ya Mipango na Utawala Bora (Administration and Good Governance /Program)
Ni Idara yenye jukumu la kusimamia shughuli zote za kiofisi ikiwa ni pamoja na masuala ya mipango na utawala bora na kufuatilia utendaji/uwajibikaji wa waratibu wote katika Wilaya.

1.3.2.      Idara ya Mafunzo na Program za Vijana (Training and Youth Program)
Idara hii ndio mhimili Wa Wilaya wa Chama. Ni Idara yenye jukumu la kuandaa Viongozi wote wa Skauti kutoka rika la Kabu, Junior, Senior hadi Rova Skauti. Idara hii ndio inayoratibu shughuli zote za progamu za Vijana na kusimamia utekelezwaji wa shughuli hizo katka makundi kwa kuzingatia “Youth Program” sambamba na kuandaa mashindano ya Skauti kwa makundi mbalimbali ngazi ya Wilaya, ikihusisha Majukwaa ya Vijana, Semina, na Warsha mbalimbali zinazohusu program za vijana Skauti. Kuandaa Watahini (Assesors) wa mashindano n.k.

1.3.3.      Idara ya Hati na Usajili (Warranty and Registration)
Idara hii ndio yenye dhamana na jukumu la kutunza na kuhifadhi kumbukumbu zote za wanachama wote wa Chama cha Skauti Wilaya ya Ubungo. Idara hii inasimamia usajili wa wanachama pamja na makundi yote ya skauti wailaya ya Ubungo sambamba na ulipaji wa ada za uanachama katika Wilaya ya Ubungo.

1.3.4. Idara ya Mawasiliano, Habari, Teknolojia na JOTA & JOTI. (ICT, and Publication)
Idara hii ndio yenye jukumu la kutunza kumbukumbu za Viongozi wote wa Skauti waliopo madarakani na ambao wamepita na kushika nyadhifa mbalimbali katika Chama. Idara hii pia inahusika kuandaa Majarida, Mikutano na Vyombo vya Habari, (Press Conferences) kurekodi Matukio mbalimbali ya Chama ngazi ya Wilaya na kuyahifadhi. Kuandaa Mafunzo ya Mawasiliano ya Radio pamoja na masuala ya ICT kwa Skauti na Viongozi wa Skauti, ikiwa ni pamoja na kuratibu na kusimamia shughuli ya kila mwaka iitwayo Jamboree ya Hewani ya Skauti (JOTA-JOTI).

1.3.4.      Idara ya Makambi na Mzingira. (Environment, Camp and Campsite )
Idara hii inahusika kulinda na kutunza Kambi za Skauti tulizonazo. Lakini kwa kushirkiana na mratibu wa shughuli za skauti ngazi ya wilaya idara hii inatakiwa kuhakikisha kuwa chama cha skauti  (W) ubungo tunakuwa na maeneo ya makambi kwa ajili ya mafunzo kwa vijana wetu wa skauti.

1.3.5.      Idara ya Hali hatarishi na Uokoaji. (Disaster Management)
Idara hii ndio inayoratibu shughuli zote za Maafa Wilayani. Inatakiwa kuandaa mpango mkakati madhubuti wa kujipanga kikamilifu katika kushiriki kwenye shughuli mbali bali za maafa zitakazo jitokeza wakati wowote lakini pia kuunda kikosi cha Vijana skauti cha maafa kitakacho kuwa tayari wakati kitapo hitajika kwa lengo la kutoa huduma.

1.3.6.      Idara ya Miradi na Maendeleo ya Jamii. (Community Development and Out Reach)
Idara hii ndio yenye kazi kubwa ya kutafuta miradi ya uzalishaji mali na kuingiza kipato kwa Chama. Ili shughuli za Chama ziweze kufanyika tunahitaji kuwa na pesa za kutosha kukidhi mahitaji ya kila Idara. Idara hii pia hutoa Mafunzo ya jinsi ya kuanzisha miradi midogo midogo kwa Makundi ya Skauti ngazi ya wilaya. Inapotokea shughuli kubwa za Chama idara hii huhusika katika kufanya fund raising mbalimbali ili kukiingizia Chama pesa.

1.4.         Idadi ya Wanachama
Hadi sasa wilaya ya Ubungo tunakadiria kuwa na wanachama zaidi ya 2,129 (Elfu mbili Mia moja Ishirini na Tisa) idadi imekuwa ikibadilika kila mwaka kutokana na wale wanao hitimu kidato cha nne na wale wanaomaliza darasa la saba kila mwaka. Pia kumekuwa na ongezeko kwa kila mwaka tunafanya usajili kwa ajili ya wanachama wapya kujiunga.

Tayari tumeshaunda mfumo malum utakaoweza kutupatia na kuhifadhi data kamili kwa Wilaya yetu ya Ubungo (Membership Database System) ambayo itaonesha idadi ya Skauti kwa makundi rika yao (Scouts Section)
Jedwali hapa chini linaonyesha idadi kwa mfumo wa rika (Scouts Section) kama ifuatavyo;-

s/n
Item
Sex
Subtotal
Total
1.      
Cub
Boys
515
1007
Girls
492
2.      
Junior
Boys
375
802
Girls
427
3.      
Senior
Boys
84
188
Girls
104
4.      
Rover
Boys
93
132
Girls
39
5.      
Grand total
2,129


1.5.         Idadi ya Wataalamu/Viongozi (Lt, Alt, Sl na Gsl)
Chama cha skauti wilaya ya Ubungo tuna makadirio ya viongozi wasio zidi 100 (mia moja) Makadirio hayo tumeyafanya kwa kupitia viongozi wanao kuja kuomba usajili wa makundi ya skaut katika wilaya yetu ya Ubungo na wale wanomba kushiriki katika kozi mbali mbali za ungozi.

Jedwali hapa chini linaonyesha idadi na ngazi zao (Scouts Rank) kama ifuatavyo;-
s/n
Item
Sex
Sub Total
Total
1.      
Lt
Male
2
2
Female
0
2.      
ALT
Male
5
6
Female
1
3.      
SL
Male
23
32
Female
9
4.      
GSL
Male
48
60
Female
12
5.      
Grand total
100


1.6. SHUKRANI
Tunashukuru uongozi mzima wa serikali wa halmashauri ya manispaa ya Ubungo yaani Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa manispaa, na maafisa elimu wote (msingi na sekondari) kwa ushirikiano mkubwa kwa Skauti.

Tunashukuru wakuu wa shule zote zenye Skauti na wazazi wa maskauti hao kwa kutuwezesha kufanya kazi zetu katika mazingira rafiki.

Tunashukuru viongozi wote wa makundi kwa jitihada na kujitoa katika kuwalea maskauti wetu.

Tunashukuru kamishna wa mkoa wa Dar es salaam na uongozi mzima wa Taifa kwa kutuonyesha dira na kutuwezesha kukamilisha majukumu yetu kikamilifu.

Mwisho lakini sio mwisho kwa umuhimu tunatoa shukrani kwa kamati ya Uendeshaji na Bodi ya wilaya ya Ubungo kwa ushirikiano, kujituma na kujitoa kwao katika kufanikisha majukumu mbali mbali.








This Blog Powerd by:
  Elbahsan Web & Blog Designer
A Subsidiary of  Elbahsan Web & Blog Designer for Global Development, Inc.
+255 (0) 653 373 432 & +255 (0) 623 511 232
For the Web & Blog Template and Designing
Dar Es Salaam, Tanzania


No comments:

Post a Comment