Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +25565373432 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Sunday, March 23, 2025

Mradi wa Elimu juu ya Afya ya Uzazi

 


Rova Skauti wilaya ya Ubungo mnamo tarehe 20/03/2025 wametembelea shule ya Sekondari Mburahati, ikiwa ni katika utekelezaji wa mikakati ya Mradi wa Elimu juu ya Afya ya Uzazi unaotekelezwa na Rova 04, Wanaowania Nishani ya Raisi. (President Scout Badge).

Mradi wa huu wa Skauti Wilaya ya Ubungo wenye lengo la Kuimarisha Afya ya Uzazi ni juhudi maalum inayolenga kuwajengea vijana uelewa na stadi za afya ya uzazi kwa lengo la kuboresha maisha yao na jamii kwa ujumla. Mradi huo, unaofadhiliwa na Africa Scout Foundation, unatekelezwa kwa kipindi cha miezi mitatu katika Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam. Uzinduzi rasmi ulifanyika katika ofisi za makao makuu ya Skauti(Upanga dsm). 


Picha ya pamoja Mara baada ya uzinduzi rasmi wa Mradi wa Elimu juu ya Afya ya Uzazi

 Darasa likiendelea wakati wa uzinduzi rasmi wa Mradi wa Elimu juu ya Afya ya Uzazi



Matukio katika picha Katika shule ya Sekondari Mburahati.

Picha ya pamoja Mara baada ya Darasa kuhusu Mradi wa Elimu juu ya Afya ya Uzazi




 Darasa likiendelea kwa wanafunzi Skauti wa Shule ya Sekondari Mburahati
kuhusu Elimu juu ya Afya ya Uzazi


No comments:

Post a Comment