Mafunzo ya Awali ya Uongozi (PTC)
Ubungo Local Scouts Association imeandaa Mafunzo ya Awali ya Uongozi (PTC). Mafunzo haya yatafanyika kuanzia tarehe 16 mpaka 19 April 2025
Mafunzo ya awali ya Uongozi wa Skauti ni mafunzo kwa ajili ya watu wazima wenye umri wa kuanzia miaka 18 (Rovers) walio tayari kujiunga au kusaidia kuendesha shughuli za Skauti kwa nyadhifa mbali mbali. Mafunzo haya yatawapa mwongozo wa kuweza kuufahamu u-Skauti na jinsi ya kuweza kusimamia na kuendesha shughuli mbali mbali za Skauti popote watakapo kuwepo.
Madhumuni ya mafunzo ya awali ni kama ifuatavyo;
1. Kupanua ufahamu kuhusu uskauti na shughuli zake.
2. Kumpatia Mshiriki stadi katika fani na mafunzo ya kiskauti.
3. Kukuza hamasa ili apende masuala ya Skauti na Chama Cha Skauti.
4. Kumhamasisha mshiriki ili aweze kuwa tayari kujituma na kujitolea katika shughuli za skauti katika wadhifa atakaopewa katika chama cha Skauti.
Mafunzo ya awali ya Uongozi wa Skauti ni mafunzo kwa ajili ya watu wazima wenye umri wa kuanzia miaka 18 (Rovers) walio tayari kujiunga au kusaidia kuendesha shughuli za Skauti kwa nyadhifa mbali mbali. Mafunzo haya yatawapa mwongozo wa kuweza kuufahamu u-Skauti na jinsi ya kuweza kusimamia na kuendesha shughuli mbali mbali za Skauti popote watakapo kuwepo.
Madhumuni ya mafunzo ya awali ni kama ifuatavyo;
1. Kupanua ufahamu kuhusu uskauti na shughuli zake.
2. Kumpatia Mshiriki stadi katika fani na mafunzo ya kiskauti.
3. Kukuza hamasa ili apende masuala ya Skauti na Chama Cha Skauti.
4. Kumhamasisha mshiriki ili aweze kuwa tayari kujituma na kujitolea katika shughuli za skauti katika wadhifa atakaopewa katika chama cha Skauti.
Mafunzo haya ni mafunzo ya maalumu kwa ajili ya watu wazima wanaotaka kusaidia kuendesha uskauti. Baada ya mafunzo haya, mshiriki anaweza kujiendeleza kwa kushiriki mafunzo ya juu zaidi ya Uongozi wa skauti ambayo yatamfanya awe kiongozi aliyefuzu yaani Skauta.
Kwa kawaida mafunzo haya huitwa mwanzo wa mafunzo ya uongozi (Preliminary Training Course) na huendeshwa kwa mtindo wa washiriki kuishi kambini kwa muda wa siku tatu au nne. Humo kambini washiriki wataishi pamoja ikiwa ni pamoja na kulala, kupika, na kula. Vilevile watashiriki shughuli zote za mafunzo wakiwa katika vikosi vya watu kati ya 6 na 8 kwa kila kikosi.
Mhitimu wa mafunzo haya hupaswa kuendesha kundi la skauti chini ya usimamizi wa Skauta kwa kipindi kisichopungua miezi sita na akipenda kujiendeleza atapaswa kuhudhuria mafunzo ya Nishani ya Skauta (Wood badge Training Course) ambayo yamegawanyika katika sehemu kuu tatu ambazo ni nadharia, kambini na vitendo.
Kiutaratibu, mafunzo haya huendeshwa na Mkufunzi yaani Leader Trainer au Mkufunzi Msaidizi ambaye huitwa Assistant Leader Trainer. Lengo la kuwatumia wakufunzi na wakufunzi wasaidizi ni kuhakikisha kuwa vipengele vyote muhimu vanatekelezwa ili kuwafanya washiriki waufahamu na kuuelewa vyema uskauti kwa nadharia na kwa vitendo.
Washiriki wanatakiwa kuthbiitisha ushiriki mapema kwa kuanza kulipia Ada (Unaruhusiwa kulipia kidogo kidogo) kabla ya tarehe 10 April 2025
Kwa Mawasiliano / Maelekezo piga au tuma SMS au WhatsApp 0747724716 | 0740222111
Imetolewa na
Idara ya Program za Vijana, Watuwazima na Mafunzo
Wilaya ya ubungo.