Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +25565373432 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Wednesday, October 2, 2019

UBUNGO PRILIMINARY TRAING COURSE


Chama cha skauti Tanzania Wilaya aya Ubungo wameandaa mafunzo ya awali ya uongozi wa skauti. Mafunzo yatafanyika kuanzia tarehe 1 hadi 4 Novemba 2019 katika eneo la Silver Sand Beach - Kunduchi. Eidha kamishna wa Skauti Wilaya ya Ubungo amesisitiza kuwa mafunzo hayo ni muhimu sana katika kuongeza idadi ya viongozi wa Skauti lakini pia kupata viongozi walio bora. Gharamaza mafunzo hayo ni Tsh 30,000/- kwa kilamshiriki, 

MADHUMUNI YA MAFUNZO:
  1. Kuwapa mbinu na uwezo wa kuratibu na kusimamia programu za skauti shuleni
  2. kujifunza mbinu za ulinzi na uslama wa mtoto, mahitaji, matarajio, changamoto wanazozikabili na jinsi ya kuzitatua.
  3. Kumfundisha mtoto dhana ya kujitolea kwa kusaidia jamii, utii, uzalendo, ujasiri, ukakamavu na utulivu kwa kupitia programu za vijana.
  4. Kutambua tabia za watoto/vijana ili waweze kuwasaidia kujirekebisha.
  5. Kuondoa tatizo la utoro, utovu wa nidhamu shuleni kwa kutumia mafunzo ya stadi za maisha.
Kasmishna wa skauti ametoa wito kwa wale wote ambao wanastahili kushiriki mafunzo hayo ikiwemo walimu walezi wa skauti mashuleni kujitokeza kwa wingi ili kupata mafunzo hayo muhimu kwa mustakbali wa  chama cha skauti na Taifa letu kwaujumla.



4 comments: